Zogo – Leo Lyrics

Zogo – Leo Lyrics

Zogo
Big up kwa Ma engineer wote,
Fundi wa Mitambo!
KD
Nishaipata Leo

Verse 1
Naipenda sana kama tende Ramadhani Naipenda sana mimi mjuukuu wa Sosoni!
Nikiikosa kweli mbele me sioni Nikiwa nayo tabasamu tu Usoni!
Nishaipata leo Sitaiwacha tena
Ni ndoto yangu naifuata fuata
Kuna vitu vingi ambavyo mimi ninataka Chukua vyote ila usninyime ndoto
Sote tunawaza juu ya siku za usoni nataka raha ye nataka shillingi 
Kama mwitaliano pindi akifika Malindi nataka joto, Yeah ninataka bibi
Na ninafanya leo Mambo mengi leo
Sijali wabishi roho juu kama simba
Kidole cha kati kati kwao na cha gumba kwao
Wote wanaoamin najua Sote tutafika

Chorus
Nishaipata leo……….

Verse 2
Kenya nzima tunataka kuishi poa tugeuke watalii wa Afrika na Ulaya
Lakini wabunge wanajali tu mishara yao, hata migingo watu waliwaachwa pekee yao
Haya kibera twende tukango’e reli
Labda baada ya hao ndipo watatusikiza
Lakini polisi watatumwa na risasi ni salamu yao toka kwa kamishna Ali
Haya wanajeshi weka mikono hewani, piga saluti weka mkono kifuani
Mko tayari simama attention toka turukana kenya nzima hadi pwani
Ndio twafanya leo Mambo mengi leo
Sijali wabishi roho juu kama simba
Kidole cha kati kati kwao na cha gumba kwao
Wote wanaoamin najua Sote tutafika

Verse 3
Naipenda sana kama tende Ramadhani Naipenda sana mimi mjuukuu wa Sosoni!
Nikiikosa kweli mbele me sioni Nikiwa nayo tabasamu tu Usoni!
Nishaipata leo Sitaiwacha tena
Nabaki safi huu ni mwanzo tafuta shillingi mwaya jasho bila shida
Napaa juu kama mawingu angani, Kila siku nayo lazima tubaki safi…

Bridge 
Na ninafanya leo Mambo mengi leo
Sijali wabishi roho juu kama simba
Kidole cha kati kati kwao na cha gumba kwao
Wote wanaoamin najua Sote tutafika

Na ninafanya leo Mambo mengi leo
Sijali wabishi roho juu kama simba
Kidole cha kati kati kwao na cha gumba kwao
Wote wanaoamin najua Sote tutafika

Chorus
Nishaipata leo……….

You cannot copy content of this page