Jemimah Thiong’o – Pendo La Ajabu lyrics

Chorus;
Yesu pendo lako ni pendo la ajabu
Yesu pendo lako ni pendo la ajabu
Yesu pendo lako ni pendo la ajabu
Pendo ambalo sikupata ulimwenguni

Verse 1:
Nilizunguka nikitafuta rafiki
Nukazunguka nikitafuta mpenzi
Rafiki wote walikuwa ni waongo
Naye mpenzi kageuka kuwa hasidi
Waliniacha nikiwa hali mahututi
Niliodhani kuwa ni rafiki zangu
Naye mpenzi akaniharibia sifa
Yesu akaja kwa kweli kaniokoa

(Chorus)

Verse 2:
Na kitandani nilikuwa nimelazwa
Marafiki wakanitazama kaenda
Wakasema kweli huyu hawezi pona
Lakini Yesu yeye hakuniacha
Korokoroni kwa kweli mi nilipofungwa
Hakuna aliyetaka kuhusishwa nami
Hakuna ndugu aliyenitembelea
Rafiki Yesu yeye hakuniacha

Verse 3:
Na isitoshe baada ya haya yote
Kanionyesha dhambi zangu huyu mpenzi
Akaniambia nikitubu taniokoa
NIweke huru kisha anipe hai
Niliopata kwa yesu ni ya ajabu
Upendo huu sijapata kuona mwingine
Sasa natangaza wote wakafahamu
Pendo la Yesu ni pendo la ajabu

(Chorus)

You cannot copy content of this page