GRA – Slow Lyrics

INTRO:
Take it ,take it, take it take it take it take it

CHORUS LYRICS:
take it take it slowly
kanyaga polepole
haraka ya maisha kutapia ukubwa wacha take it slow×2

VERSE 1 LYRICS:
usichague uzuri wa ndizi kwa kukagua maganda
nasema usini jaji kwa ninazo vaa pamba
kwa kuwa sija gonga headlines haimaanishi unidharau
jaribu kuskiza vina ndo unilinganishe nao
napenda sana wanapobana akili inakomaa roho inakuwa ngumu sana
nakataa tamaa za ujana eti puf puf kiasi ndo niweze kuwaza sana
hakuna hesabu isiyo na jibu kwanza isome ramani afu maujanja taratibu
mvumilivu hula mbivu vitabu ndo viliandikwa
zangu nkipata mbichi sijali nazifundika
nifuateni hamtapotea ntawaongoza mi ni compas sio kama secondary michano yangu ndo campus
usiniite superstar niite wako shujaa
nimepitia kwenye moto ka dhahabu ndo nang’aa
G_R_A so versatility,quality music nakupa kitu reality hakuna muda wa kujaribu wee fanya kama unaweza mambo yakiwa shkopa na kamba usije legeza
sija fika ninapokwenda ila nahisi niko very close
fikra potov G_R_A ndo nawa brainwash

CHORUS LYRICS:
take it take it slowly kanyaga polepole haraka ya maisha kutapia ukubwa wacha take it slow×2

VERSE 2 LYRICS:
wacheni nianze kwa maombi nipeni yangu tasbi
ni baada ya kuthawadha niondoe nasji
huno uislamu wa kweli sio kwa kanzu nyeupe
ni kwa mema maadili ndo ukimwomba mola akupe ukiweza kusaidia wee toa mia kwa mia
na upatapo msaada wagawie wenzako pia
haijalishi wapi umetoka
bora uwe na nia na kufeli usije ogopa
usilalame hauna cash jaribu kupata mkopo
kwani ukosefu wa wajenzi una maana wingi wa mikoko wingi wa maneno sio uzito wa busara
bora ubaki kimya au upayuke tukwite fala
siulizi mengi maswali mi ni sehemu ya jawabu
ukinielewa mambo shwari ukini puuza haina tabu
lipiza ubaya wa adui kwa mengi mambo mema
wee jifanye kama haujui moyo wake ndo unauchoma ulipewa mdomo mmoja na maskio mawili
ili uskize zangu hoja afu uchunge zako kauli
mwanzo wa starehe ndo mwisho wa mafanikio ukipenda sana kupare mwishoni huwaga kilio
usiku wee kunywa pombe asubuhi hangover chupa za ngano ugonge mfukoni gameover

CHORUS LYRICS:
take it take it slowly kanyaga polepole haraka ya maisha kutapia ukubwa wacha take it slow×2

BRIDGE LYRICS:
bandua mguu twende pamoja take it slow twende pamoja bandua mguu twende pamoja take it take it take it slow
bandua mguu twende pamoja wacha haraka ya maisha bandua mguu twende pamoja na take it take it slooow

CHORUS LYRICS:
take it take it slowly kanyaga polepole haraka ya maisha kutapia ukubwa wacha take it slow×2

OUTRO:
from chocolate city (malindi) to all over the world… G_R_A ON THIS ONE. g ra. ma man eazy!!!

You cannot copy content of this page