Gabriel Omollo – Lunchtime Lyrics

sasa ni lunchtime
tufunge makazi
twende kwa chakula
tuje tena saa nane

wengine wanakwenda
kulala uwanjani
kumbe ni shida ndugu
njaa inamwumiza

wengine wanakunywa
soda na keki
huku roho yote
kwa chapati na ng’ombe

na wengine nao wazunguka maduka
huku wakijidai
wanafanya window shopping

kufika mwisho wa mwezi
uwanja thire mundu
ukiona anayelala
pia asiye na kazi

wamekwenda wote
kula hotelini
wengine kwa biriani
wengine kuku na wali

watu wa Industrial Area
watoroka maharagwe
waenda hotelini
kwa chapati na ng’ombe

na wengine nao
wale mishahara juu
siku hiyo wote
kwa hoteli za wazungu

kumbe shida ndio hufanya
mtu kulala chini ya miti
kumbe shida ndio hufanya
mtu kung’ang’ana na maharagwe
kumbe shida ndio hufanya
mtu kuonekana kama mtoto
nimeelewa eeh, nimeelewa oh
nimejua kumbe ni shida oh
nimeelewa eeh, nimeelewa oh
nimejua kumbe ni shida oh

kumbe shida ndio hufanya
mtu kulala chini ya miti
kumbe shida ndio hufanya
mtu kung’ang’ana na maharagwe
kumbe shida ndio hufanya
mtu kuonekana kama mtoto
nimeelewa eeh, nimeelewa oh
nimejua kumbe ni shida oh
nimeelewa eeh, nimeelewa oh
nimejua kumbe ni shida oh

You cannot copy content of this page