Eric Wainaina – Nchi ya kitu kidogo Lyrics

Verse 1
Mzee alisema hakuna cha bure
Huo msema tumeutafsiri kinyume
Hata shule kuiingiza mtoto
Lazima utoe mchoto
Kupata simu ni balaa
Road license bei nafuu utanunua
Kupoteza ID ni mashaka
Twaarudisha Jamhuri yetu nyuma

Chorus
Nchi ya kitu kidogo
ni nchi ya watu wadogo

Ukitaka chai ewe ndugu nenda Limuru

Verse 2
Hata nyumbani ukipatwa na majambazi
Kupiga 999 wasema, ‘Sisi hatuna gari
Lete elfu tano ya petroli, saidia utumishi’
Mahakamani hela ndio haki
Kwa elfu chache mshtakiwa ndiwe mshtaki
Ushahidi hwa utajiri
Twarudisha Jamhuri yetu nyuma jamani

Chorus
Nchi ya kitu kidogo
ni nchi ya watu wadogo
Ukitaka soda ewe Inspekta burudika na Fanta
Nchi ya kitu kidogo
ni nchi ya watu wadogo
Ukitaka chai ewe Mama nunua Ketepa

Verse 3
Huko Kenyatta madawa zimeisha
Mas**ti zauzwa marikiti mia kwa mia
Wafanyi kazi waenda miezi bil pesa
Ni bahati ukitibiwa
Mzigo wetu nazidi kuwa mzito
Watoto wanne na mshahara wa elfu mbili mia tano
Ya viatu, ya vitabu na vyakula
Nauliza na Mbotela
‘Je, huu ni ungwana?’

Chorus
Nchi ya kitu kidogo
Ni nchi ya watu wadogo
Ukitaka chai ewe ndugu nenda Limuru

You cannot copy content of this page