Eric Wainaina Featuring MC Kah – Fungeni Macho Lyrics

Verse 1
Tulifunga macho kuomba
Tuliibiwa ardhi
Bendera ya Mungu ilipeperuka
Mwafrika akikaa kwa imani
Cheupe kilijiuza
Cheusi kilifukuzwa
Tuliambiwa,˜Imbeni alleluia.
Fungeni macho imbeni.


Chorus
Tumegongwa tumeamka
Tumekanyagwa tumejitoa
Tumelazwa tumesimama heye!
Tumebanwa tumeepuka
Kusulubiwa tumeshuka
Tumeuawa tumefufuka aye!


Verse 2
Mwaka wa 1963
Tulijishindia Uhuru
Bendera ya Mzungu iliteremshwa
Mwafrika alianza kujitawala
Tuliambiwa, ˜Harambee! Harambee!
Furuteni mzigo.
Tuliambiwa Fuata Nyayo!
Fungeni macho fuata Nyayo!


Chorus
Tumegongwa tumeamka
Tumekanyagwa tumejitoa
Tumelazwa tumesimama heye!
Tumebanwa tumeepuka
Kusulubiwa tumeshuka
Tumeuawa tumefufuka aye!


Verse 3
Na bado twangoja wokovu
Twangalia milimani
Twauliza mwokozi ni nani
Twafaa kutazama kiooni
Kila mmoja ni kiongozi
Kila mmoja ni mwalimu
Kila mmoja ni mjenzi
Kila mmoja achukue madaraka

You cannot copy content of this page